Staa wa zamani wa Chelsea ya England na Real Madrid ya Hispania Michael Essien March 14 2017 ametangaza kujiunga rasmi na timu ya Persib Bandung ya Indonesia baada ya kuwa nje ya uwanja bila timu kwa miezi sita.
Essien alikuwa hana timu kwa kipindi cha miezi sita baada ya kuachana na Panathinaikos ya Ugiriki mwaka 2016 na amekuwa akifanya mazoezi na kikosi cha akiba cha Chelsea kabla ya kujiunga na Persib Bandung.
Michael Essien mwenye umri wa miaka 34 alikataa kujiunga na Melbourne ya Australia mwezi December mwaka jana, Essien amewahi kuichezea Chelsea ya England kwa misimu nane.
image
Wednesday 15 March 2017
New
Baada ya kuwa nje ya uwanja ndani ya miezi sita Essien amepata Timu
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment