Wednesday 15 March 2017

Kilichoendelea Leo Mahakamani Kuhusu Kesi ya Madawa ya Kulevya Inayomkabili Wema Sepetu


Kesi ya Dawa za kulevya inayomkabili muigizaji wa filamu nchini Tanzania, Wema Sepetu iliyokuwa isikilizwe leo, imeahirishwa hadi Aprili 11 mwaka huu baada ya upande wa mashtaka kudai kuwa upelelezi haujakamilika.

Muigizaji huyo ni mmoja kati ya wasanii ambao walitajwa kwenye list ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda yawatuhumiwa wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Katika upelelezi wa awali ambao ulifanywa na jeshi la polisi, walidai wamekuta msokoto wa bangi nyumbani kwa muigizaji huyo.

No comments:

Post a Comment